Construction Documents Muhimu kwa Site Engineer/Technician katika Kusimamia Miradi ya Ujenzi.

Pata picha unataka kwenda mahali ambapo haupajui na hauna muongozo.? 💭

Unadhani utafika vipi labda.? Na itakuchukua muda gani na gharama kiasi gani kufika hapo mahali eti..

Basi hivyo ndivyo ilivyo ukiwa kama site engineer au technician unasimamia mradi bila kuwa na construction documents..


Kabla hujaendelea kusoma makala hii zaidi naomba usapoti channel yangu ya YouTube ==> HAPA hii inanitia moyo kuendelea kuandaa makala zenye kukupa mwanga kama hizi...🙏👍

Kwenye makala hii utaenda kujifunza construction documents  muhimu kwa Site Engineer/Technician katika kusimamia miradi ya ujenzi.

Je, Construction Documents ni nini.?

Hizi ni legally binded contract documents muhimu ambazo zinaelezea kwa usahihi jinsi mradi (construction project) itakavyojengwa: materials unazohitaji, kiwango cha materials na kiwango cha kazi kinachotakiwa, ramani ya mradi na vipengele vyake vyote.

Baada ya kuomba mradi kama mkandarasi na ukaupata basi kuwa na kupewa construction documents ni lazima na ni muhimu mno kwa sababu hizi ndizo muongozo wako wawe kufanya unachotaka kukifanya na clients wakitaka kukulipa na kupima utendaji wako wa kazi wanatumia hizi construction documents.

Hizi ndio construction documents  muhimu kwa Site Engineer/Technician katika kusimamia miradi ya ujenzi ;-

  • Working Drawings
  • Bill of Quantities
  • Specifications

1. Working Drawing

Baada ya mradi wowote ule kuwa designed uwe ni  mradi wa daraja, culvert, jengo, barabara, tenki la maji, mfumo wa maji safi, n.k lazima designer atoe michoro.

Michoro ndio kitu pekee kinachokuwezesha wewe kama site engineer/technician kutimiza lengo la designer.

Mchoro ndio kitu kinachokupa picha halisi wewe unatakiwa ufanye kitu cha aina gani, kiweje na kiwe na muonekano upi.

Working drawing ndio blueprint (map) ya kukuwezesha wewe kufika unakotaka kufika, kufanya ujenzi unaotaka kuufanya.

Hauwezi kusimamia mradi kiusahihi bila kuwa na mchoro, itakuwa ni kitu ch ajabu mno wewe kama msimamizi wa site na haujui umuhimu wa michoro..

Working drawing zinatakiwa ziwe zionyeshe detail kwa upande wa Plan, Section na Elevation.

Plan view inaonyesha muonekana uliokamilika kwa upande wa juu..

Elevation inaonyesha muonekana uliokamalika kwa upande wa kulia, kushoto, nyuma na mbele.

Section inaonyesha detail za ndani zote na vipimo vyake.

Kazi nyingine za working drawings ni ;-

  • Kukusaidia kupata vibali vya ujenzi
  • Kukusaidia kuaanda B.O.Q
  • Kukusaidia kuandaa specification
  • Kukusaidia kwenye tendering stage

    2. Bill of Quantities (B.O.Q)

    B.O.Q inakusaidia wakati wa kuomba mradi kujaza rate na bei utakazo tumia kufanya huo mradi.

    B.O.Q ndio muongozo wako wakati wa utendaji na usimamiaji wa mradi inakupa mwanga na picha kujua kama kazi unayofanya wakati huu umeifanya kwa hasara au faida.

    B.O.Q pia inakupa nafasi ya kuandaa working schedule na schedule of Materials.

    B.O.Q ndio reference wakati wa malipo... It's very absurd kwa site engineer au technician kuniambia unasimamia mradi na hauna B.O.Q au huja isoma B.O.Q vizuri na kuilewa ni kitu cha ajabu you know..😬😬.

    3. Specifications

    Specifications ndio documents ya tatu muhimu unayohitaji wakati unasimamia mradi site engineer/ technician.

    Specification inakupa muongozo wa materials unazohitaji kwenye mradi, kiwango na ubor wa kazi unahohitajika.

    Usichangenye mambo hapo specification na B.O.Q ni vitu viwili tofauti.

    Na hizi ndizo  Construction Documents  Muhimu kwa Site Engineer/Technician katika Kusimamia Miradi ya Ujenzi.

    Kupata sample ya hizi construction documents zote bofya ==> HAPA

    Soma makala nyingine hizi kujifunza zaidi.. 


      Previous Post Next Post

      Contact Form