📘 Program Maisha Baada ya Chuo Kama Civil Engineer/Technician
Program Hii Ni Maalum Kwa Wahitimu Watarajiwa Civil Engineers/Technicians TU!
Kupitia Program Hii Utaenda Kupata Majibu ya Maswali yote yanayokutatiza na Kukunyima RAHA kama Mhitimu Mtarajiwa Kada ya Civil Engineering Ngazi ya (Diploma au Bachelor) Kila Unapowaza Maisha Baada ya Kumaliza Chuo Kama:
- Nitaanzia wapi baada ya kumaliza chuo, kabla sijaajiriwa na sina mtaji?
- Nitaanzia wapi kutengeneza pesa baada ya kumaliza chuo?
- Jinsi ya kutumia elimu yako ya kitaalamu ya "Civil Engineering" kujikwamua kiuchumi.
- Msingi wa kujiajiri moja kwa moja ikiwa ajira za makampuni binafsi na serikali zitakuwa changamoto.
- Nitapata vipi "connections" zitakazonisaidia kupata kazi?
- Jinsi ya kujenga uzoefu utakao kusaidia kupata kazi katika makampuni makubwa.
- Vitu gani vitakavyomfanya mhitimu wa Civil Engineering aweze kuendesha mradi mpaka mwisho kwa ufanisi?
- Itachukua muda gani kujiajiri au kupata ajira kama Civil Engineer/Technician?
- Je, nianze kufanya kazi inayohusiana na taaluma yangu ya Civil Engineering au kazi yeyote itakayopatikana kwa wakati huo?
- Nitaanzaje au nitaanzia wapi kuishi na kufanya kazi katika taaluma yangu ya Civil Engineering?
- Baada ya kumaliza chuo, nitawezaje kupata fursa za kuendeleza taaluma yangu kabla sijapata ajira?
- Tofauti zilizopo kati ya kufanya kazi kwa mkandarasi, Kujiajiri na kuajiriwa serikalini kama “Civil Engineer/Technician”.
- Ni changamoto gani zipo kwenye soko la ajira kwa sasa?
Au ni mara yako ya kwanza kuchagulia katika interview TAMISEMI upande wa
engineering & construction na hauelewi uanzie wapi 😕😕.?
Kama ni hivyo basi hii makala ipo kwa ajili yako, kabla hatujaendelea
naomba chukua muda wako kidogo sapoti channel yangu ya YouTube bofya
==> HAPA 🙏
Pia unaweza kupitia makala hizi kujifunza zaidi;
- Top 50 TANROADS interview question and answers for weighbridge shift-in charge and operator.
- Top 50 most asked TANROADS interview question and answers for civil technician and engineers.
- Je, Civil technician ana majukumu gani site? Kazi na majukumu 10 ya civil technician site.
Katika interview zaidi ya tano za UTUMISHI upande wa engineering &
construction nilizokuwa shortlisted na kufanikiwa kuudhuria zaidi ya 60%
nilifanikiwa kufika mpaka oral interview.
Unajaribu kutafakari nilizingatia hasa mambo gani.? 💭
Haya ndio mambo makuu matatu nilizozingatia yaliyoniwezesha kupata
mafanikio hayo.
Jambo la kwanza: Elewa majukumu (responsibilities) zote za kazi uliyoiombaa na taasisi uliyoomba majukumu yake kiutendaji.
Ile ujiandae vizuri na interview yoyote ya UTUMISHI upande wa engineering
& construction, jambo la kwanza kabisa unalotakiwa kulijua kwa undani ni
kujua na kufahamu majukumu ya kazi uliyoomba na sekta uliyoomba inahusika na
kazi gani hasa kiutendaji.
Mfano:
Kazi uliyoomba - Technician (Civil) - II
- To inspect and reports on roads and bridge maintenance works
- To supervise road and bridge maintenance works
- To measure and certifies works for payment
- To undertake road inventory and condition survey
- To undertake road traffic count
- To carry out in situ testing
- To undertake laboratory tests and to monitor tests results and trends
- To prepare invoices for materials testing
- To undertake laboratory apparatus and equipment calibration
- To prepare site report and
- To perform such other related duties as may be assigned by the Supervisor.
Taasisi - TANROADS
Majukumu makuu ya taasisi hiyo ni
- Road and hydraulic structures construction
- Road and hydraulic structures maintenance
- Weighbridges Operation Services
- Advise/work together with other Road authorities
Kupitia mfano huo jua hapo unapata picha kwamba interview yako ita base
hasa upande gani.?😉😉
Jibu => Ni upande wa barabara na miundo mbinu yake.
Jambo la pili : Jua modules zote ulizosoma chuoni zinazohusiana au kushabiiana na jibu ulilolipata hapo juu kwenye jambo la kwanza.
Baada ya kufahamu na kujua majukumu yako na majukumu ya kiutendaji makuu ya
taasisi yako.
Kinachofata ni kureview masomo yote uliyoyasoma chuoni, references na manual zote zinazoshabiiana na jibu ulilolipata kwenye kwenye jambo la kwanza
juu pale.
Jibu tuliolipata juu pale interview yetu ita base haswa upande wa barabara
na miundo mbinu yake kwaio sehemu kubwa unazotakiwa kupitia na kufanya
review moja ni module zote ulizosoma chuoni zinazohusiana na ilo ambazo
ni:
- Road construction and maintenance
- Pavement design and construction
- Road geometry design
- Bridge design & construction
- Design of hydraulic structures
- Highway materials
- Surveying
- Pavement and Material Design Manual 1999
- Road Geometric Design Manual 2012
- Tanzania Field Testing Manual 2003
- Laboratory Testing Manual 2000
- Standard Specification for Road Works 2000
- Low Volume Road Manual 2016
!! ... Usizime moto 🔥🔥 ili kupata matokeo ..😊😊
Jambo la tatu : Kama ukifanikiwa kufika Oral interview.
Kama umefanya jambo la kwanza na la pili kwa usahihi zaidi jambo la tatu ni
rahisi tu kama kusukuma mlevi 😃😃 kwa sababu asilimia 75% ya maswali
utakuwa na uwezo wa kuyajibu.
Unatakiwa tu kuzingatia muda eneo la usahili.
Ukiwa ndani ya chumba cha usahili relax ukiulizwa maswali jibu kwa utulivu,
taratibu usiwe na haraka epuka kuongea haraka haraka jiamini.
La mwisho sehemu iliyobaki MUACHIE MUNGU...🙏🙏 wewe kama mwanadamu
hivo jua hapo ndio vitu unavyoweza kufanya vyote ndani ya uwezo wako.
Hitimisho hayo ndio mambo 3 muhimu ya kuzingatia ili kufanikiwa kwenye
interview za engineering & construction - UTUMISHI
Kama umenufaika na makala hii comment & share ili
iwasaidie na wengine.
Kama umenufaika na makala hii naomba muda wako mchache kusapoti channel
yangu ya youtube bofya ==>
HAPA
Kuona fursa mbalimbali za kazi engineering & construction bofya =>
HAPA
Kupata reference books & manual bofya =>
HAPA