📘 Program Maisha Baada ya Chuo Kama Civil Engineer/Technician
Program Hii Ni Maalum Kwa Wahitimu Watarajiwa Civil Engineers/Technicians TU!
Kupitia Program Hii Utaenda Kupata Majibu ya Maswali yote yanayokutatiza na Kukunyima RAHA kama Mhitimu Mtarajiwa Kada ya Civil Engineering Ngazi ya (Diploma au Bachelor) Kila Unapowaza Maisha Baada ya Kumaliza Chuo Kama:
- Nitaanzia wapi baada ya kumaliza chuo, kabla sijaajiriwa na sina mtaji?
- Nitaanzia wapi kutengeneza pesa baada ya kumaliza chuo?
- Jinsi ya kutumia elimu yako ya kitaalamu ya "Civil Engineering" kujikwamua kiuchumi.
- Msingi wa kujiajiri moja kwa moja ikiwa ajira za makampuni binafsi na serikali zitakuwa changamoto.
- Nitapata vipi "connections" zitakazonisaidia kupata kazi?
- Jinsi ya kujenga uzoefu utakao kusaidia kupata kazi katika makampuni makubwa.
- Vitu gani vitakavyomfanya mhitimu wa Civil Engineering aweze kuendesha mradi mpaka mwisho kwa ufanisi?
- Itachukua muda gani kujiajiri au kupata ajira kama Civil Engineer/Technician?
- Je, nianze kufanya kazi inayohusiana na taaluma yangu ya Civil Engineering au kazi yeyote itakayopatikana kwa wakati huo?
- Nitaanzaje au nitaanzia wapi kuishi na kufanya kazi katika taaluma yangu ya Civil Engineering?
- Baada ya kumaliza chuo, nitawezaje kupata fursa za kuendeleza taaluma yangu kabla sijapata ajira?
- Tofauti zilizopo kati ya kufanya kazi kwa mkandarasi, Kujiajiri na kuajiriwa serikalini kama “Civil Engineer/Technician”.
- Ni changamoto gani zipo kwenye soko la ajira kwa sasa?
Asilimia nyingi ya vitu tunavyosoma tukiwa chuoni ni theory (nadharia) na
sehemu ndogo tu ndio practical.
Kiasi mtu anapomaliza masomo anakuwa hafahamu ujuzi gani hasa.?? 👀
utamsaidia kupambana na kazi za site.
Kabla ujaendelea kusoma makala hii naomba muda wako kidogo sapoti chaneli
yangu ya YouTube bofya ==>
HAPA
hii inanipa moyo na faraja mimi kukuandalia makala za kujifunza kama
hizi.
Pia unaweza kupitia makala hizi kujifunza zaidi;
- Fahamu mambo 3 muhimu ya kuzingatia ili kufanikiwa kwenye interview za engineering & construction -TAMISEMI
- Je, Civil technician ana majukumu gani site? Kazi na majukumu 10 ya civil technician site.
- Top 50 TANROADS interview question and answers for weighbridge shift-in charge and operator.
- Top 50 most asked TANROADS interview question and answers for civil technician and engineers.
Tunaendelea. . . .
- Videfca Construction & Technical Services Ltd
- Maclesence Investment Company Limited
- Mtwivila Traders & Construction Company Ltd
- Hano Construction Company Limited n.k
Siku ya kwanza nimefika tu nikapelekwa site hafu hata nnachotakiwa
kukifanya site nilikuwa sijui ni nini..😆🙈 najua utakuwa unapata picha
kama hiyo na maanisha nini hapo..💭💭 mafundi wanategemea maelezo kutoka
kwako hafu na wewe hujui chochote
Kuna site nyingine nilijikuta mimi ndio msimamizi na meneja wa kila
kitu lakini hata pakuanzia nilikuwa sijui ni wapi.?😫😫
Hii yote ni kutokana nilikuwa sifahamu aina za ujuzi ambao ungekuwa ni
msaada kwangu kusimamia site ila baada ya muda nilikuja kufahamu skills
nilizokuwa nahitaji ili kusimamia site kwa mafanikio.
Kwa utafiti uliofanya na watu fulani hizi ndizo aina kuu 5 za ujuzi
unaohitaji wewe kama civil site engineer/technician na asilimia za
uhitaji wake ili uwe tayari kusimamia kazi site.
[Image credit: digiqc - (source: https://www.digiqc.com)]
1. Kusoma michoro ya kazi site (Working drawing Interpretation) - (90.4%)
Kama inavyofahamika lugha ya wahandisi ni mchoro..😊
Huwezi kufanya kazi yoyote ile kama hujaelewa mchoro, kusoma mchoro
ni zaidi ya asilimia 40% ya kufanyika kwa kazi.
Majibu ya mchoro ndio yanatoa muongozo wa vitu vingine vyote
kufanyika kama setting out, excavation n.k
Kama hujui kusoma mchoro huwezi kujua kama ulichofanya ndio
kinachotakiwa au siyo.
Na hamna mradi au kazi ya civil engineering inayofanyika bila mchoro
(working drawing), mchoro ndio base line yakukuongoza wewe na hata
client/consultancy atakupima kulingana na mchoro ulivyo na unavyolipwa
utalipwa kulingana na vipimo vya mchoro.
Unachotakiwa kama ni msimamizi wa barabara tafuta michoro mingi kadri
uwezavyo na ujifunze kuisoma, kama ni majengo pia vivyo hivyo
n.k..
2. Kufatilia na kujua ubora wa kazi na material site (Quality check and
control) - (72.1%)
Ili ufanye kazi ya site kwa ubora lazima ujue kuzingatia ubora wa
material zinazotumika na kazi unayoifanya.
Na kitu kinachokupa muongozo hapa ni specifications na standard code
zinazohitajika kwa ajili ya kazi.
Kwaio kama ni unasimamia kazi ya barabara lazima ujue vizuri
specifications zote za material yanayohitaji na kazi inayohitajika
kisha uzingatie hivyo katika utendaji.
Cha muhimu hapa ni kusoma specifications na standard code uzijue in
and out..💪
3.Setting out, surveying & levelling - (58.7%)
Hakuna structure inayojengwa hewani 😀😀
Baada ya kuweza kusoma mchoro lazima ujue kile kilichopo kwenye
mchoro unakiamisha vipi kikae ardhini..😄
Hapa ndiopo umuhimu wa kujua setting out, line out, staking,
surveying na levelling unapokuja
Vibarua kazi yao ni kufata maelekezo yako kwamba ichi kina kaa hivi
ichi hivi n.k
Lazima ulijue ili, ili kuweza kusimamia kazi yako site.
4. Kufanya makadirio ya kazi na gharama (Quantity estimations) - (49%)
Ili ujenzi na kazi ya site iendelee utahitajika kufanya ordering ya
material kwaio lazima ujue kuandaa schedule of material, kufanya
makadirio ya viwango vya materials vinavyohitajika na gharama zake ili
uiingiliwe wala kufanya kazi kwa hasara.
Ujuzi huu unasaidia pia hata katika work valuation, lazima ujue kupima
na kufanya measurements za kazi yako site uweze kulipa vibarua, mafundi
lakini pia hata wewe kulipwa
5. Usalama mahali pa kazi (Safety matters) - (40.4%)
Asilimia takribani 15% za ajali zinazotokea duniani zinatokana na
ujenzi kwaio lazima ulifahamu ilo na kulisimamia kwa sababu OSHA wanapiga faini usipokuwa makini kwaio wewe kama msimamizi wa site ilo
ni muhimu kulijua.
Kwaio ujuzi kuhusu usalama wa kazi ni kitu muhimu mno mno.
Kwaio unatakiwa kumkumbusha kuvaa vifaa kinga kama reflectors, safety
boots, elements ili kuepukana na ajari za site.
Simamia profesional yako inavyotakiwa💪💪usionekane mbabaishaji, site
engineer/technician...!!
Hitimisho hizo ndio aina kuu tano (5) za ujuzi muhimu unaotakiwa
kuwa nao civil site engineer/technician ili kusimamia na kumeneji
kazi site.
Kama umenufaika na makala hii usisahau kuweka comment yako & share ili iwasaidie na wengine... 🙏🙏
Pia naomba muda wako mchache kusapoti channel yangu ya youtube
bofya ==> HAPA
Fursa mbalimbali za kazi engineering & construction bofya
==> HAPA
Kupata specifications & manual bofya ==> HAPA
Kupata schedules of material, BOQ na excelsheets bofya ==>
HAPA
Kupata SEAP reports bofya ==> HAPA
Kama una swali lolote tuwasiliane email:
tony.mbugi@must.ac.tz
I appreciate you sir
ReplyDelete