📘 Program Maisha Baada ya Chuo Kama Civil Engineer/Technician
Program Hii Ni Maalum Kwa Wahitimu Watarajiwa Civil Engineers/Technicians TU!
Kupitia Program Hii Utaenda Kupata Majibu ya Maswali yote yanayokutatiza na Kukunyima RAHA kama Mhitimu Mtarajiwa Kada ya Civil Engineering Ngazi ya (Diploma au Bachelor) Kila Unapowaza Maisha Baada ya Kumaliza Chuo Kama:
- Nitaanzia wapi baada ya kumaliza chuo, kabla sijaajiriwa na sina mtaji?
- Nitaanzia wapi kutengeneza pesa baada ya kumaliza chuo?
- Jinsi ya kutumia elimu yako ya kitaalamu ya "Civil Engineering" kujikwamua kiuchumi.
- Msingi wa kujiajiri moja kwa moja ikiwa ajira za makampuni binafsi na serikali zitakuwa changamoto.
- Nitapata vipi "connections" zitakazonisaidia kupata kazi?
- Jinsi ya kujenga uzoefu utakao kusaidia kupata kazi katika makampuni makubwa.
- Vitu gani vitakavyomfanya mhitimu wa Civil Engineering aweze kuendesha mradi mpaka mwisho kwa ufanisi?
- Itachukua muda gani kujiajiri au kupata ajira kama Civil Engineer/Technician?
- Je, nianze kufanya kazi inayohusiana na taaluma yangu ya Civil Engineering au kazi yeyote itakayopatikana kwa wakati huo?
- Nitaanzaje au nitaanzia wapi kuishi na kufanya kazi katika taaluma yangu ya Civil Engineering?
- Baada ya kumaliza chuo, nitawezaje kupata fursa za kuendeleza taaluma yangu kabla sijapata ajira?
- Tofauti zilizopo kati ya kufanya kazi kwa mkandarasi, Kujiajiri na kuajiriwa serikalini kama “Civil Engineer/Technician”.
- Ni changamoto gani zipo kwenye soko la ajira kwa sasa?
Nakumbuka kipindi fulani wakati nasimamia mradi wa barabara (Upgrading of Hotelitatu-Mkazambo Road Kilwa District to Gravel Standard) kama site engineer, nilipelekwa borrowpit nikaonyeshwa material mahali pa kuchukua kifusi na layman mmoja hivi nikawa sijui nimwambie operator aanze kuchukua kifusi wapi na wapi aache.?😠
Yule layman akawa kama ndio msemaje mkuu sasa ana muongoza operator mimi nikiwa nashindwa kujua kama kifusi kinafaa au laah nikawa najiuliza mimi kama site engineer kazi yangu ni nini endapo layman ndio mtoa maamuzi, yeye alichokuwa anasema tu kwamba kinatumika ichi ichi kifusi miaka yote..
Kuna wakati hadi nikawa naona mbona kama operator anakataa kifusi ambacho ni vumbi kabisa niliduawa mno ila layman yule akawa anasimama kwamba tunatumia hicho hicho, hiyo yote ni kwa sababu nilikuwa nakosa technical skills za site (upande wa materials) yaani kama nikiwa site naweza kujua kwamba haya material yanafaa kwa ajili ya gravel wearing layer au laah.!!
Kwenye makala hii utajifunza essential technical skills ambazo ni muhimu mno kwako kama site engineer na technician ili kusimamia mradi wowote bila changamoto..
Hizi ndizo essential technical skills za site ambazo kila site engineer na technician ili kusimamia mradi wowote bila changamoto.
1. Kusoma na kutumia standard codes and specifications wakati wa usimamizi.
Hamna mradi wa ujenzi unaofanyika bila kufata specification na standard
code (miongozo ya kazi), kila nchi ina miongozo yake kwenye ujenzi
(construction) kwaio hata hapa nchini kwetu tuna miongozo inayotusaidia sisi
katika kusimamia na kufanya kazi mbalimbali
TARURA wana muongozo wao unaowasaidi katika kusimamia na kutenda kazi, TANROAD vivyo hivyo, National Irrigation Commision (NIC) waona muongozo kwa ajili ya utendaji wa kazi zao, Halmashauri n.k
2. Road Geometric Design Manual 2012
3. Tanzania Field Testing Manual 2003
4. Laboratory Testing Manual 2000
5. Standard Specification for Road Works 2000
6. Low Volume Road Manual 2016
2. Materials and material testing.
Ufahamu na ujuzi wa site kuhusiana na material (kokoto, mchanga, mawe,
matofari) kuna miradi unatasimamia ambayo haihitaji test za material za
mahabara ila wewe kama site engineer au technician lazima ujue je kama hayo
material yatafaa kwa ujenzi au laah,
Na hichi ndicho kilichonikuta mimi nilikuwa sifahamu kifusi gani kinafaa kwa matumizi site kwa kukiangalia tu.
3. Estimation and Costing.
Lazima uwe unajua kufanya makadirio ya kazi (upande wa material na kazi) na
gharama, kuna muda utatakiwa ku order material kutoka mbali na kwa gharama
ya jua kwaio kama ukiwa una hesabu mbovu itakula kwako.
Kuna muda utasimamia kazi inayotumia mitambo ya kukodi kwaio usipokuwa na makidirio sahihi utajipiga pini..💪
Kwaio huu ni essential skills mno mno wewe kama site supervisor...✌✌
4. Quality control.
Unaposimamia site kuna kazi mbalimbali utazisimamia ikiwa zege, formwork, stone masonry, stone pitching n.k na zote lazima zifanyike katika ubora kwaio kusimamia kiwango cha kazi ni skills muhimu mno, kwa sababu usipokuwa makini utajikuta unaingiza hasara kwa kurudi kazi au kupata kashfa ya kusimamia mradi usiokuwa na viwango.
5. Kutumia vifaa mbalimbali vya survey.
Vifaa kama levelling machine, Total station, Tape measure unatakiwa ujue namna ya kutumia kwa sababu utakuwa site utatakiwa kupima, kuset level ili kazi iendelee..
6. Drawing and design.
Baada ya kazi kuishi utahitajika kuandaa michoro inaitwa A built drawing.
Kwaio skills za drawing and design ni muhimu kwako the big boss..
7. On field management.
Mhandisi nakupa mbinu zingatia haya..!!
Kama umejifunza kitu share na marafiki zaidi ili wajifunze.!
Kujifunza zaidi pitia makala hizi zaidi:-